Somo la Kwanza: Dan 9:4–10
Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na
rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake; tumefanya dhambi, tumefanya
ukaidi, tumetenda maovu, tumeasi, naam, hata kwa kuyaacha maagizo yako na
hukumu zako; wala hatukuwasikiliza watumishi wako, manabii,
ambao kwa jina lako
walisema na wafalme wetu, na wakuu wetu, na baba zetu, na watu wote wa nchi. Ee
Bwana, haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna haya ya uso, kama hivi leo; kwa
watu wa Yuda, na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa Israeli wote, walio karibu
na hao walio mbali, katika nchi zote ulikowafukuza, kwa sababu ya makosa yao
waliyokukosa. Ee Bwana, kwetu sisi kuna haya ya uso, kwa wafalme wetu, na wakuu
wetu, na baba zetu, kwa sababu tumekutenda dhambi. Rehema na msamaha ni kwa
Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi; wala hatukuitii sauti ya Bwana, Mungu wetu,
kwa kwenda katika sheria zake, alizoziweka mbele yetu kwa kinywa cha watumishi
wake, manabii.
Wimbo wa Katikati: Zab 79:8–9, 11, 13
Usikumbuke juu yetu maovu ya baba zetu, Rehema zako zije kutulaki hima, Kwa maana tumedhilika sana.
Injili:Lk 6:36:38
Yesu aliwaambia wafuasi wake: Iweni na huruma, kama Baba
yenu alivyo na huruma. Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi
hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa. Wapeni watu kitu, nanyi mtapewa;
kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu
watakachowapa vifruani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho
mtakachopimiwa.
No comments:
Post a Comment