Tafakari ya Neno la Mungu, Jumatatu 2/3/2020
Somo la
Kwanza: Law. 19:1-2,11-18
1BWANA akanena na Musa,
akamwambia, 2Nena na mkutano wote wa wana wa Israeli,
uwaambie, Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi BWANA, Mungu wenu, ni mtakatifu. 11Msiibe, wala msidanganye, wala msiambiane uongo. 12Msiape uongo kwa jina langu, hata ukalinajisi
jina la Mungu wako; Mimi ndimi BWANA. 13Usimdhulumu jirani yako, wala kumnyang’anya mali
yake; ijara yake aliyeajiriwa isikae kwako usiku kucha hata asubuhi. 14Usimlaani kiziwi, wala usitie kwazo mbele ya
kipofu, bali umche Mungu wako; Mimi ndimi BWANA. 15Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee
mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu; bali utamhukumu jirani yako kwa haki. 16Usiende huko na huko katikati ya watu wako, kama
mchongezi; wala usisimame kinyume cha damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA. 17Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima
kumkemea jirani yako, wala usichukue dhambi kwa ajili yake. 18Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya
wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA
Wimbo
wa katikati: Zab19:7-9,14
Bwana
unayo maneno ya uzima wa milele
Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake,
na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha
utukufu wake; 32na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye
atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; 33atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi
mkono wake wa kushoto. 34Kisha
Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba
yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; 35kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula;
nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; 36nalikuwa
uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni,
mkanijia. 37Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana,
ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha? 38Tena
ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika? 39Ni
lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia? 40Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia,
kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea
mimi. 41Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa
kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa
tayari Ibilisi na malaika zake; 42kwa
maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe; 43nalikuwa
mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na
kifungoni, msije kunitazama. 44Ndipo
hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una
kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie? 45Naye
atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao
walio wadogo, hamkunitendea mimi. 46Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya
milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.
1BWANA akanena na Musa,
akamwambia, 2Nena na mkutano wote wa wana wa Israeli,
uwaambie, Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi BWANA, Mungu wenu, ni mtakatifu. 11Msiibe, wala msidanganye, wala msiambiane uongo. 12Msiape uongo kwa jina langu, hata ukalinajisi
jina la Mungu wako; Mimi ndimi BWANA. 13Usimdhulumu jirani yako, wala kumnyang’anya mali
yake; ijara yake aliyeajiriwa isikae kwako usiku kucha hata asubuhi. 14Usimlaani kiziwi, wala usitie kwazo mbele ya
kipofu, bali umche Mungu wako; Mimi ndimi BWANA. 15Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee
mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu; bali utamhukumu jirani yako kwa haki. 16Usiende huko na huko katikati ya watu wako, kama
mchongezi; wala usisimame kinyume cha damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA. 17Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima
kumkemea jirani yako, wala usichukue dhambi kwa ajili yake. 18Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya
wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA
Wimbo
wa katikati: Zab19:7-9,14
Bwana
unayo maneno ya uzima wa milele
Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake,
na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha
utukufu wake; 32na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye
atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; 33atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi
mkono wake wa kushoto. 34Kisha
Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba
yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; 35kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula;
nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; 36nalikuwa
uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni,
mkanijia. 37Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana,
ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha? 38Tena
ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika? 39Ni
lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia? 40Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia,
kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea
mimi. 41Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa
kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa
tayari Ibilisi na malaika zake; 42kwa
maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe; 43nalikuwa
mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na
kifungoni, msije kunitazama. 44Ndipo
hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una
kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie? 45Naye
atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao
walio wadogo, hamkunitendea mimi. 46Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya
milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment