Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili 1/3/2020
Somo la
Kwanza: Mwa 2:7-9,3:1-7
BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi,
akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. 8BWANA Mungu akapanda bustani upande wa mashariki
wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya. 9BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti
unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya
bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Basi
nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya BWANA Mungu.
Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti
yote ya bustani? 2Mwanamke
akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; 3lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani
Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. 4Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, 5kwa
maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa
macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. 6Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa
chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa
katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. 7Wakafumbuliwa
macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini,
wakajifanyia nguo
wimbo
wa katikati: zab 51:1-4,10-12,15
Uturehemu,ee
Bwana, kwa kuwa umetenda dhambi
Somo la
Pili: Rum.5:12-19
Injili
: Mt. 4:1-11
Kisha Yesu alipandishwa na Roho
nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi. 2Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho
akaona njaa. 3Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe
haya yawe mikate. 4Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila
neno litokalo katika kinywa cha Mungu. 5Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu,
akamweka juu ya kinara cha hekalu, 6akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini;
kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua;Usije
ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu
Bwana Mungu wako. 8Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote
za ulimwengu, na fahari yake, 9akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka
kunisujudia. 10Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa,
Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 11Kisha Ibilisi
akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.
BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi,
akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. 8BWANA Mungu akapanda bustani upande wa mashariki
wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya. 9BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti
unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya
bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Basi
nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya BWANA Mungu.
Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti
yote ya bustani? 2Mwanamke
akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; 3lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani
Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. 4Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, 5kwa
maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa
macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. 6Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa
chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa
katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. 7Wakafumbuliwa
macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini,
wakajifanyia nguo
wimbo
wa katikati: zab 51:1-4,10-12,15
Uturehemu,ee
Bwana, kwa kuwa umetenda dhambi
Somo la
Pili: Rum.5:12-19
Injili
: Mt. 4:1-11
Kisha Yesu alipandishwa na Roho
nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi. 2Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho
akaona njaa. 3Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe
haya yawe mikate. 4Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila
neno litokalo katika kinywa cha Mungu. 5Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu,
akamweka juu ya kinara cha hekalu, 6akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini;
kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua;Usije
ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu
Bwana Mungu wako. 8Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote
za ulimwengu, na fahari yake, 9akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka
kunisujudia. 10Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa,
Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 11Kisha Ibilisi
akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment