Musa aliwaambia watu: Leo hivi akuamuru Bwana, Mungu wako,
kuzifanya amri hizi na hukumu; basi uzishike na kuzifanya kwa moyo wako wote na
roho yako yote.Umemwungama Bwana leo, kuwa ndiye Mungu wako, na kuwa yakupasa
kutembea katika njia zake, na kushika amri zake na maagizo
yake, na hukumu
zake, na kusikiza sauti yake; naye Bwana amekuungama hivi leo kuwa taifa
iliyotengwa iwe yake yeye, kama alivyokuahidi, na kuwa yakupasa kushika maagizo
yake yote; na kuwa atakutukuza juu ya mataifa yote aliyoyafanya kwa sifa, na
jina na heshima, nawe upate kuwa taifa takatifu kwa Bwana Mungu wako, kama
alivyosema.Wimbo wa katikati : Zab 119:1-2, 4-5, 7-8
Injili : Mt 5:43-48
Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Mmesikia kwamba imenenwa,
Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; lakini mimi nawaambia, Wapendeni
adui zenu, waombeeni wanaowaudhi; ili mpate kuwa wana wa Baba yetu aliye
mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye
haki na wasio haki. Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi, mwapata thawabu? Hata
watoza ushuru; je! Nao hawafanyi yay ohayo? Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu,
mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama
hayo? Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo
mkamilifu.
No comments:
Post a Comment